Showing posts with label poverty. Show all posts
Showing posts with label poverty. Show all posts

Friday, June 18, 2010

Scientific research and society - a lecture by Kofi Annan

Theme: Scientific Research and Society
Venue
: Swiss Federal Institute of Technology (ETH) - Zurich, Switzerland

Today I was fortunate enough to attend an overbooked lecture by Mr. Kofi Annan, the former UN-SG and Nobel Peace Prize Laureate. For this year's Richard R. Ernst Lecture at the ETH Zurich, Mr. Annan delivered a captivating lecture on the role of scientific research in solving the needs of society . He urged young researchers to delve into research that crosses boundaries of their fields through interdisciplinary work and international collaborations with less technological advanced nations. Addressing a multitude of young researchers and students, Mr. Annan pointed out that scientists should provide the necessary leadership in research policy when political support is lacking. This could be through creating innovative solutions to societal needs that gain public support of the target communties. He pressed on the need of academics to refuse to remain in the ivory-tower, but rather become actors through research that makes a lasting impact to society. During the lecture, he quoted the Indian statesman and foremost actor in its R&D revolution, Jawaharlal Nehru, who once said "we are too poor to not invest in science and technology", to highlight the importance of science and technology for solving incessant problems of the south - food shortage, climate change and diseases of poverty.

The full lecture

(c) ETH Zurich, ITS-MMS

Below are amateur video clips of the panel discussion with Kofi Annan chaired by the 1991 Chemistry Nobel Laureate Prof. Richard R. Ernst.





Darwin's Nightmare

A 2004 documentary film written and directed by Hubert Sauper -- dealing with the environmental and social effects of the fishing industry around Lake Victoria in Tanzania.



Quote from the Darwin Nightmare's website:

"Some time in the 1960's, in the heart of Africa, a new animal was introduced into Lake Victoria as a little scientific experiment. The Nile Perch, a voracious predator, extinguished almost the entire stock of the native fish species. However, the new fish multiplied so fast, that its white fillets are today exported all around the world.

"Huge hulking ex-Soviet cargo planes come daily to collect the latest catch in exchange for their southbound cargo… Kalashnikovs and ammunitions for the uncounted wars in the dark center of the continent..."

Sunday, June 13, 2010

Uvumbuzi mahsusi kwa walemavu


Amos Winter, mwanafunzi wa shahada ya uzamivu pale MIT, Marekani yuko njiani kuwekeza matokeo ya elimu yake katika kusaidia walemavu wa nchi maskini. Winter ametengeneza wheelchair maalum kwa walemavu wa miguu kwa ajili ya matumizi kwenye barabara zilizo na mabonde au matope tulizonazo 'uswahilini'. Mradi wake huo uitwao, Leverage Freedom Chair, umemwezesha kushinda tuzo mbalimbali pamoja na kuweza kufundisha wanafunzi wengine kuhusu teknolojia hii. Wenzetu wa VETA na SIDO, mpoo?






Tembelea ukurasa wake hapa ili kufahamu zaidi kuhusu kazi zake.

Tuesday, June 8, 2010

Watanzania na Ujio wa Brazil



Kipyenga cha mwisho kimelia, huku Brazil wakishinda mpambano dhidi ya Taifa Stars kwa magoli matano kwa moja. Mazungumzo na mabishano juu ya mechi hii iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na Watanzania wengi itabaki kuwa gumzo la jiji kama sio nchi, kwa wiki kadhaa zijazo. Watanzania tutaelekeza nguvu zetu kwenye kupiga domo juu ya mechi hii huko vijiweni kabla ya hali halisi ya maisha yetu duni kutuzindua kwenye starehe hii iliyo dumu kwa dakika 90.

Ujio wa Brazil umepokelewa kwa hisia tofauti, wengi wakishabikia kuwa hatimaye watamwona mchezaji mahiri wa Brazil, KaKa kwa macho yao wenyewe. Kuna kundi dogo la watu waliotaka Watanzania tususie mechi kwani haina manufaa yoyote katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu. Zogo hili la ujio wa Brazil lilianza kupaa kwa kasi pale Bw Paulo Kamau wa Kenya alipobeza uamuzi huu wa Tanzania kuwalipa fedha nyingi vijana hao wa Samba.

Tanzania Football Federation (TFF) wamekuwa kimya kuzungumzia kiwango halisi walichowapa Brazil, wakati mwazoni walidai kuwa Serikali iliwatengea fungu la dola za Kimarekani milioni sita. Tovuti ya BBC wamedai kuwa TFF iliwalipa dola milioni mbili na nusu. Kiasi taslimu cha fedha walicholipwa Brazil bado kinabaki kuwa tata, huku Raisi wa TFF ndugu Leodegar Tenga akidai kuwa, "It's definitely that the coming of top players in the world will be a big boost to local football as well as the tourism sector,".

TFF imejitetea kuwa, ujio wa Brazil utachochea maendeleo katika soka na kwenye sekta ya utalii. Hizi ndizo sababu kuu mbili zakutetea matumizi makubwa ya fedha ya kuwalipa Brazil kuja kucheza na Taifa Stars, sasa swali ni hili, Je Tenga na TFF wana hoja ya msingi?

Mimi binafsi sidhani kama hoja hiyo ina nguvu ya kutosha kuhalalisha matumizi ya hivyo vijisenti walivyowalipa Brazil, na hoja zangu ni kama ifuatavyo. Soka la Tanzania limekuwa kichwa cha mwendawazimu kwa miaka mingi, na mimi nina uhakika wengi tunajua ni nini kinatakiwa kufanyika ili kuinua soka la Tanzania. Tatizo la kwanza, tunapenda kukimbia kabla hatujajua kutembea, na hoja hii aliizungumzia kocha wa Taifa Stars wa sasa ndugu Marcio Maximo alipotoa ushauri wake juu ya soka la Bongo. Mimi sio mtaalamu saana wa soka wala sijawahi kuwa kwenye kamati ya ufundi wa tunguli, lakini hoja ya Maximo itaungwa mkono na wengi wenye uwerevu. Watanzania inatubidi tuanze kujenga utamaduni wa kusikiliza wataalamu na sio wanasiasa wasio jua lolote.

Sasa tukija kwenye sababu ya pili, ya kuwa ujio wa Brazil utasaidia soko la utalii, nadhani kuna mambo kadhaa ya kuangalia kwa utaratibu. Jambo la kwanza, tuna uhakika gani ujio wao utaongeza ujio wa watalii? Najua moja ya jibu la swali hili litakuwa, kwasababu mechi inaonyeshwa moja moja katika nchi zisizopungua mia 160. Hii inaweza saidia; lakini wasiwasi wangu ni kuwa, kuna utafiti mdogo umefanywa katika kuhakikisha kuwa hii ndio njia bora ya kutangaza nchi yetu. Katika mpango huo, je tuliangalia njia mbadala ambazo zingetugharimu fedha kidogo zaidi na ambazo tungekuwa na uhakika zaidi kuwa zitazaa matunda?

Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Shamsa Selengai Mwangunga (MB) alipotoa makadirio ya Wizara yake Bungeni, aliongelea mipango kadhaa ya Wizara yake. Moja ya mipango hiyo ilikuwa ni kuongeza utalii wa ndani, kwa kuwapunguzia Watanzania viingilio katika mbuga za wanyama na sehemu nyingine za kitalii. Mkakati huo ni mzuri, lakini bado tunategemea zaidi watalii wa nje. Lakini kidogo kimefanyika kuhamasisha watalii wa nje kuja nchini. Tanzania bado inatajwa kama nchi yenye viwango vikubwa (fees) kwa watalii, ukilinganisha na Kenya na Uganda. Kenya na Uganda walipunguza viwango vyao baada ya uchumi wa dunia kuyumba, lakini Tanzania bado tumeacha viwango vikiwa juu. Sasa hapo ndio kuna mgongano wa mawazo -- huku tunatumia mamilioni kadhaa kutangaza nchi, lakini hatupunguzi viwango. Hao watalii wataishia kwenda Kenya na Uganda na kukwepa Tanzania, hivyo mwisho wa siku tunajaza maji kwenye pekecha.

Ripoti ya Repoa iliyokuwa inazungumzia The Role of Tourism in Poverty Alleviation in Tanzania ni ripoti inayotoa mapendekezo yakinifu. Pamoja na ripoti hiyo iliyotoka miaka saba iliyopita, lakini mapendekezo yake bado yana umuhimu, sasa sijui mapendekezo mangapi ya ripoti hiyo yalifanyiwa kazi na Serikali kupitia Wizara yake husika. Mimi nakubali sekta ya utalii inaumuhimu mkubwa, hasa katika kuchangia kupunguza umasikini. Lakini je, tumeboresha sekta hiyo kwa kiasi gani? Tanzania leo tunaweza kusema huduma zetu za utalii zinaweza kushindana na nchi nyingine za Afrika au bado huduma zetu ni duni. Miundombinu bado ni tatizo kubwa, lakini tumeng’ang’ania kutangaza nchi. Jamani, akili ya namna hii haina tofauti na akili ya mtu anayekaribisha wageni kabla ya kufagia nyumba na kuhakikisha kila kitu kiko sawa.

Timu ya Brazil nd’o hiyo imekuja na kuondoka, sasa ningependa kuona kama malengo ya mpango huo yatafikiwa; soka ya bongo kuhamasika na hao watalii kuongezeka. Mimi kwa kiasi fulani ninakubaliana na baadhi ya watu waliotaka Watanzania tususie mechi hiyo na pia ninakubaliana kwa kiasi fulani na mawazo ya Kamau. Tanzania ni nchi masikini kutumbua fedha zote hizo kwenye kitu ambacho hatuna uhakika kitalipa. Tanzania tukiwa kama nchi moja masikini sana duniani, lazima tuwekeze fedha za walalahoi kwenye mambo ya msingi zaidi, sio kwenye starehe za dakika mbili tatu. Majuzi tu, tulikuwa wenyeji wa mkutano wa uchumi wa dunia. Ukiniuliza mimi hiyo ilikuwa nafasi nzuri kutangaza nchi. Je, tulifanya hivyo ipasavyo, au tulishangalia tu wageni waliokuja?

Aliyesema ng’ombe wa masikini hazai, hakukosea. Na msemo huu ni kweli kwani, ni watu masikini ambao mara nyingi hufanya maamuzi ya papara bila kufikiria kuwa kuna kesho. Tuendelee kuzungumzia ni jinsi gani Brazil walivyopigwa chenga na Taifa Stars, lakini wao haoooo wanaelekea kwenye Kombe la Dunia, Sisi je? Kamau alivyozungumzia “character” yetu Watanzania hakukosea sana. Pamoja simuungi mkono na kejeli zake, lakini alikuwa na hoja. Hivi kweli watu wazima tunaweza kusema,” tumefungwa lakini tuliwapiga chenga”. Hilo ni jambo la kushabikia kweli? Tukiendelea na akili hizo sisi kila siku tutanyonywa na kukandamizwa kwani tumekuwa watu wa kufurahia mafanikio madogo, tena ya kijinga, badala ya kusimama na kupigania maendeleo makubwa yenye maana. Tumezidi kuwa wa ndio mzee, badala ya kuuliza maswali, kupigania haki zetu na kupigani uwajibishwaji wa viongozi wabovu wenye kunuka ufisadi. Watanzania, hivi ndio tumekubali kuwa umasikini ni utamaduni wetu?

Watanzania wenzangu waliojitutumua na kulipa viwango vikubwa kuwaona Brazil, je, ulifikiria mechi hiyo kama ina manufaa kwa nchi yetu. Hivi ni wewe huyo huyo unayelalamika kuwa barabara zimechakaa na msongamano wa magari umekithiri. Wewe ulilipa kwenda kumwangalia KaKa, je nyumbani kwako haupatagi matatizo ya kukatiwa maji na umeme mara kwa mara au unajenerata na bwana la maji nyumbani? Leo hii ukalipe fedha zote hizo kuwaona Brazil, alafu kesho unafanya kila uwezalo kukwepa kulipa kodi na kupokea rushwa. Watanzania tunazungumzia sana kuhusu tulivyo masikini, lakini hapo hapo tunataka starehe zinazotushinda uwezo. Naona tunataka kulazimisha maji yachanganyike na mafuta; kweli Tanzania tuna akili zinazotutosha sisi wenyewe.

Ushauri wangu ni huu, kama tulivyopigania tiketi za kumwona KaKa, basi moyo huo huo wa kupigana usiishie hapo. Moyo huo uendelee katika kupigania maendeleo, kupinga viongozi wabovu, tuwe na kiu ya maendeleo na ari ya kuchapa kazi kama tulivyoshangilia magoli ya Brazil kwa nguvu zetu zote. Tuache kuendeshwa na hisia bali tuendeshwe na fikra, kwani ujio wa timu ya Brazil hauwiani na msemo wa ‘mgeni njoo wenyeji tupone’, bali ni ‘mgeni njoo wenyeji tuzidi kuumia’. Mimi ninawatakia kila la kheri Brazil kwenye kombe la dunia na sisi kama kawaida yetu tutaishia kulishangalia kwenye runinga, kama utamaduni wetu, kwani sisi ni nambali moja kwa kushangalia maendeleo ya wengine na kuiga mambo yasiyo na manufaa.

Picha kwa hisani ya cartoonist Gado

Saturday, June 5, 2010

Tovuti ya Wahapahapa Na Sanaa..



Leo hii sanaa bado haijapewa heshima na kipaumbele kama inavyotakiwa, pamoja na sanaa kuwa kioo cha jamii. Tovuti na blog zimeanza kumea kama uyoga, lakini chache zimekuwa zikitetea nafasi ya sanaa katika jamii na haki na umuhimu wa wasanii ndani ya jamii.

Wahapahapa ni moja ya tovuti ninazoweza kusema zimejikita katika sanaa, siyo kuishia kuzungumzia sanaa tu. Kitu kilichonifurahisha na tovuti ya wahapahapa, ni kuwa wameweka michezo ya kuigiza ya redio katika tovuti yao. Hii inawapa fursa hata walio mbali kufaidi sanaa hii kongwe iliyopewa kisogo kutokana na ukuaji wa utandawazi. Nadhani kizazi cha enzi zile tunaweza kukumbuka ile michezo ya akina marehemu Pwagu na Pwaguzi katika redio ya Taifa, RTD.

Tembelea tovuti hii ya Wahapahapa na sikiliza michezo hiyo ya kuigiza na pia kujisomea mambo mengi mengineo ya kuelimisha kupitia sanaa.

Friday, June 4, 2010

11 minutes on Poverty

by Lars Johansson (with English subtittles)

Video clips from six Maweni Farm documentaries from Tanzania, Kenya and Nigeria, prepared for Sida (2008).


Ziwa Viktoria - Mgongowazi

Na Lars Johansson (with English subtittles)

Ufuatao ni mkusanyiko wa filamu fupi kadhaa wa mambo yanayotokea kwenye vijiji vilivyopo karibu na Ziwa Viktoria. Mradi huu uliofanywa mwaka 2004 ni wa Maweni Farm na IOGT.


Tuesday, May 25, 2010

Tanzania ni Nchi ya Wapole

Mzazi: We Sikuzani, embu acha hiyo!

Mtoto: Kwanini!?

Mzazi: Kwasababu nimesema!

Haya ndio yaweza kuwa majibizano mafupi katika familia nyingi tulizokulia. Mtoto hapewi nafasi ya kujibiwa swali lake, na mara nyingi majibu yatolewayo ni ya ukali au ya kuonyesha utawala. Mara nyingine ukiuliza 'kwanini', unaweza kubalazwa kofi, kwasababu tu umemjibu mzazi!

Nimeamua kugusia mada hii muhimu ya malezi baada ya kusoma kitabu cha Annette Lareau kiitwacho Unequal Childhoods: Class, Race, and Family Life. Kitabu hiki kinatoa mwanga kuhusu tofauti za malezi zilizopo kati ya familia zenye kipato kikubwa/kawaida (mtaani tutaziita za 'geti kali') na zile za kipato cha chini ('uswazi'), yaani middle-class vs. working-class parenting. Muandishi amejaribu pia kueleza ni sifa gani zinawasaidia au kuwaathiri ukubwani watoto kutokana na tofauti ya malezi kati ya matabaka haya mawili. Ingawa tafiti ya kitabu hiki inahusu familia za marekani, kwa kiasi fulani mengi tunaweza kujifunza kuhusu mazingira ya malezi tuliyonayo Tanzania na jinsi gani tunajenga taifa potofu la wapole.


Lareau anaanza kwa kueleza tofauti mbili za malezi: malezi aina ya concerted cultivation (yanayofuatwa na wale wa 'geti kali') na ya accomplishment of natural growth (yanayofuatwa na wa kipato cha chini). Tofauti kati ya aina hizi ya malezi nitaziainisha hivi punde.

Ili kufahamu tofauti zilizopo katika aina hizi ya malezi, Lareau alifanya mahojiano na wanafunzi zaidi ya 80 wa darasa la tatu na nne kutoka familia za wamarekani weusi pamoja na wazungu. Katika kipindi cha utafiti wake, aliweza kubainisha kuwa aina ya malezi ya watoto inategemea na kipato (tabaka) cha (la) familia, wakati kabila (race) ya familia haina uhusiano wowote.

Kwenye malezi ya concerted cultivation aligundua kuwa, wazazi hawa wengi ni wa kisomo cha juu. Wazazi hawa wanahusika mno katika malezi ya watoto wao nyumbani na kwa kiasi kikubwa pia katika shughuli zao nje ya nyumba (kama ufuatiliaji wa maendeleo yao ndani na nje ya darasa). Wazazi wanashughulikia kuwatafutia na kuwaandikisha wanao katika shughuli za nje ya darasa zinazohitaji usimamizi wa wakubwa, mfano: uskauti, mafunzo ya kuogelea, mafunzo ya kupiga kinanda, n.k. Nia yao ikiwa kuwasaidia watoto wao wawe all-rounded ili kupata ujuzi zitakazowasaidia katika maisha ya ukubwani – hasa hasa katika kazi za utaalamu (white collar jobs). Pia, wazazi hawa mara nyingi walikuwa tayari kuingilia kati pindi kukitokea tatizo shuleni kuhusu watoto wao, pamoja na kukutana na walimu wa shule kuulizia maendeleo yao.

Pamoja na hayo, mazingira ya wanayokulia watoto hawa nyumbani ni tofauti (sio kifedha, bali kijamii). Laureau, anaeleza kuwa wazazi katika familia hizi wanajihusisha zaidi kuongea na wanao, na hivyo kuwasaidia watoto kukuza vocabulary au hata ari yao kujiamini. Ari hii ya kujiamini, inakuzwa kwani wazazi pia wanawahimiza wanao kuuliza maswali au ku’negotiate na wakubwa ipasavyo. Pia, amri zinazotoka kwa wazazi huwa zinaambatanishwa na maelezo ya kwanini wanatoa amri hizo. Hivyo, watoto hawa wanakuwa na mazoea mapema ya kuongea na wakubwa na kujua namna ya kujieleza (mf. matumizi ya eye contact), na hata kuwa na uwezo wa kujieleza mbele ya umati. Kumbuka watoto waliofuatiliwa ni wa umri wa miaka kati ya 7 na 9. Laureau anaeleza kuwa, 'ubaya' wa malezi haya ulionekana kwa ukithiri wa watoto kulalamika-lalamika ovyo, kutaka kuwa centre of attention, kuwa wabishi/watundu, kimbelembele, kutojua umuhimu wa pesa, pamoja na kutokuwa karibu na ndugu/koo.

Wazazi wa familia zenye kipato cha chini walifuata aina ya malezi ya accomplishment of natural growth. Katika malezi haya, mzazi hajihusishi mno katika dunia ya mtoto zaidi ya kutoa chakula, malazi, elimu, na mavazi. Tumaini la wengi wa wazazi hawa ni kwamba mtoto atakuwa (atapevuka) tu, sponteaneously – yaani, 'muache mtoto awe mtoto'. Lareau anaandika kuwa, watoto wa malezi haya muda wao mwingi baada ya shule hutumia kucheza na wenzao na hawana ratiba iliyobana ya extracurricular activities kama waliokuwa nayo wa 'geti kali'. Katika malezi haya mazingira au ‘dunia’ ya nyumbani ya mtoto na mzazi ina mipaka thabiti. Mzazi hajihusishi kwa kiasi kikubwa na kazi za mtoto za nyumbani, na mara nyingi wazazi wanatoa amri/adhabu kwa wanao bila hata kumueleza mtoto ‘kwanini’ (mf. Sikuzani na mzazi). Hivyo, watoto wanakuwa na woga kujieleza kwa mamlaka (watu wazima), na mara nyingi wanakuwa na heshima binafsi ndogo (self-esteem). Uzuri wa malezi haya yanafahamika na wengi, kwani katika jamii ya nchi yetu ni aina hii ya malezi inafatwa. Sifa chanya ni kama watoto wanakuja kuwa wakarimu/diplomatic, waangalifu katika masuala ya pesa, n.k.

Lareau anaonya kuwa, hakuna mzazi mbaya au mzuri. Ila, malezi ya concerted cultivation yanawapa advantage fulani watoto ukubwani, hasa katika utafutaji wa kazi (job market). Baada ya miaka 15, Lareau alifuatilia maendeleo ya watoto hawa ili kufahamu wanajihusisha na nini. Watoto waliokulia malezi ya concerted cultivation (geti kali) wengi wao wanafanya kazi katika kazi za utaalam (white collar jobs), wakati wengi wa waliolelewa kulingana na modeli ya accomplishment of natural growth walikuwa bado wanabangaiza.

Mara ngapi umemuuliza mtoto swali dogo tu mtaani, na akaficha uso/mdomo na kukujibu kwa kunong'oneza, hii kama hajakupa jibu: "sijui"? Kwanini watoto wengi (hasa wasichana) Tanzania wanakula chakula chumba tofauti na baba mwenye nyumba?

Nchini Tanzania ni aina ya malezi ya accomplishment of natural growth yanayofuatwa na wengi. Hii inachangiwa sana na hali ya umaskini (mfano: mzazi hajui kusoma/kuandika), ila kwa namna kubwa inachangiwa na mila/desturi zetu tulizorithi kutoka mababu. Ni muhimu kutafakari kuwa mila na desturi hizi nyingi hazitatupa advantage yeyote katika dunia ya sasa na kesho ambayo vijana wachakarikaji wanahitajika. Hali ya umasikini wetu kwa namna moja au nyingine inatokana na aina ya malezi tunayokuza watoto wetu.

Jinsi dunia inavyozidi kuwa competitive, ndivyo tunavyotakiwa nasi kubadilika na kujenga taifa la vijana wanaojiamini walio na umahiri wa kuchukua nafasi katika kila anga. Tunahitaji wananchi wasioogopa kuuliza maswali kwa viongozi wao, hivyo wasio rahisi kudanganywa uchaguzi baada ya uchaguzi. Wananchi wa aina hii ndio wasioogopa kuleta mapinduzi katika jamii ili kufuta status quo. Wananchi wa aina hii tutawapata kama tukiwalea watoto wetu kupitia malezi ya concerted cultivation. Ni hivi tu, tutapata wafanyabiashara mahiri, professionals chungu nzima, na muhimu zaidi raia wawajibikaji. We need less submissive citizens and more of whom are ready to take charge.

Nimechoka kusikia kutoka kwa wageni kuwa: “watanzania ni wapole”.

Ningependa kumaliza kwa kumnukuu David Brooks: “todays rich don’t exploit the poor, they outcompete them.”


picha:

http://www.worldvision.org.uk/server.php?show=nav.201

http://imaginationlane.blogspot.com/2010/04/masai-children.html