Monday, June 7, 2010

Kama chenga tu, tumewala

Tanzania 1 - 5 Brazil (Highlights)



Leo tufurahie chenga za Ngassa na goli la Aziz. Kesho tunaanza kuuliza maswali -- vipi ilikuwaje uwanja haukujaa? Hela za kuwalipa zilipatikana wapi? Faida n.k.

7 comments:

  1. huyu kipa ni nani?na imeuaje akachezeshwa?

    ReplyDelete
  2. nyabe...chenga tu tumewala..ngassa kifaa...tatizo kipa....ni nani yule?why him?hawezi hata kutembea, hana timing na mpira....yaani dah!!

    ReplyDelete
  3. Mnakumbuka enzi zile tulipokuwa tunasema kipa/beki hasifiwi? Sasa haya ndio matatizo yake ukubwani... Watu wachache sana wanatilia maanani kuwa beki mzuri au kipa bora wakata wanaanza kucheza mpira.

    Huu ni mjadala wa siku nyingine. Yule ndio kipa wetu na ile ndio defence yetu.

    ReplyDelete
  4. haha aisee..bora hata na beki SN kipa haijelewi kabisa...lakini kuna funzo pale..am sure tuki rematch bila yule kipa mambo yatakua mengine!!
    cousin

    ReplyDelete
  5. Cousin, wewe ni binamu ninayemfahamu? Nadhani kama wewe ungekaa golini labda tungefungwa 2-1 tu.

    ReplyDelete
  6. Mrudisheni Kaseja golini, Chuji, Humud na Boban wapeni dimba. Kwenye ushambuliaji sina wasiwasi kama dimba litachukuliwa na vijana wa kazi.

    ReplyDelete
  7. Hahahaa! tunajifunza au tunajaribu sikuelewa mchezo wa wachezaji wa Tanzania kumng'ang'ania kumkaba Kaka au mlifikiri kamera zinamulika mwenyewe na wengine ni Underground? Tupige kabumbu tuache majigambo

    ReplyDelete