Showing posts with label Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Tanzania. Show all posts

Friday, June 18, 2010

Darwin's Nightmare

A 2004 documentary film written and directed by Hubert Sauper -- dealing with the environmental and social effects of the fishing industry around Lake Victoria in Tanzania.



Quote from the Darwin Nightmare's website:

"Some time in the 1960's, in the heart of Africa, a new animal was introduced into Lake Victoria as a little scientific experiment. The Nile Perch, a voracious predator, extinguished almost the entire stock of the native fish species. However, the new fish multiplied so fast, that its white fillets are today exported all around the world.

"Huge hulking ex-Soviet cargo planes come daily to collect the latest catch in exchange for their southbound cargo… Kalashnikovs and ammunitions for the uncounted wars in the dark center of the continent..."

Wednesday, June 16, 2010

TAMASHA-Vijana na Ujamaa Hip Hop Darasa

Ukiperuzi haraka haraka kwenye hii makala unaweza ukadhani umepotea njia na uko kwenye blog ya Fid Q. Hapana -- hapa ni Vijana FM, mzee!

Kama nilivyosema wiki chache zilizopita, kuna baadhi ya mambo au harakati zinazofanywa na Vijana wenzetu ambazo mara nyingi hazitambuliwi; kwa maneno mengine, inaonekana hazipewi kipaumbele. Lakini nadhani Vijana FM itabadili hii desturi.

Nia hasa sio tu kuwafagilia tu Vijana wenzetu. Ni matumaini yangu kuwa makala kama hizi zitawapa wahusika changamoto na kuwahamasisha Vijana wengine kujiunga na kuwasaidia wahusika kwa namna moja au nyingine.

Leo hii nakuletea harakati za Winston Churchill na timu yake nzima ya TAMASHA-Vijana. Mchana wa leo (tarehe 16 Juni, 2010) ulikuwa ni maalumu kwa ajili ya Watoto wa Afrika, na mzee mzima Fid Q ndio alikuwa mgeni rasmi au mwalimu wa kwanza wa Ujamaa Hip Hop Darasa.

Kabla sijakupa dondoo za hili Darasa, ningependa kukuambia madhumuni hasa ya TAMASHA-Vijana/Ujamaa Hip Hop Darasa.

Winston anasema,"[Tunajitahidi] kufikiria jinsi ya kuwasaidia Vijana... maana tunaona wana vipaji lakini jinsi ya kuvibadili katika ujasiriamali bado imekuwa ndio changamoto. "

Kwahiyo wameamua kuanzisha Ujamaa Hip Hop Darasa. Hili Darasa litakuwa linatumia falsafa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere: "Binadamu hujikomboa na kujiendeleza mwenyewe; hawezi kukombolewa na kuendelezwa." Na litakuwa linatumia taswira ya utamaduni wa Ujamaa wa Kiafrika na Hip Hop ili kuwavutia zaidi Vijana.

Darasa rasmi la kwanza la Hip Hop litaanza tarehe 26 Juni (Mikocheni, Old Bagamoyo Rd, Dar es Salaam). Licha ya kwamba Madarasa yatakuwa bure, waandaji bado wanafikiria namna ya kufanya mpangilio mzima uweze kujiendesha wenyewe.

Ukiacha Hip Hop Darasa kuna mambo mengine yatakayokuwa yanaendelea na kufanyiwa kazi -- kwa mfano, utengenezaji wa video (Research, Archive and Documentary on Hip Hop), Outreach and Relations, Uhuru Clothing na Film Project.

Napenda kuchukua fursa hii kuwatakia kila la kheri TAMASHA-Vijana na Ujamaa Hip Hop Darasa kwenye shughuli zao na nadhani timu ya Vijana FM itajaribu kuwasaidia pale itakapoweza.

Cha muhimu zaidi ni wasanii wengine, wataalamu wa mambo haya na Vijana kwa ujumla kuitikia mwito.

Nawatakia jioni njema!

Tuesday, June 15, 2010

African Hip Hop Thesis

Mimi kama mpenzi mkubwa wa Hip Hop, nimekuwa nikijaribu kuifuatilia kwa karibu tangia '2 Proud' alipokuwa anavuma na nyimbo kama 'Ni mimi, niko kwenye maikrofoni' na 'Madawa ya kulevya'. Safari ya Hip Hop Tanzania ni ndefu kiasi chake -- ila wengi mtakubaliana na mimi kuwa hatuna "kioo" (as in, standard) madhubuti cha kuangalia na kutath'mini mabadiliko yaliyoletwa na huu muziki wetu.

Mara nyingi mambo mengi tunayojadili kuhusu Hip Hop tunakuwa kama tuna speculate tu. Kwahiyo, tunayoongelea kwenye kijiwe hiki ni tofauti na yatakayoongelewa kwenye kijiwe kingine kutokana na sababu kadhaa.

Fid Q nadhani ameliona hilo na ameamua kufanya utafiti kuangalia Hip Hop kutoka Afrika -- utafiti huu wa kitaaluma utachunguza nini hasa kinachotokea kwenye ulingo wa Hip Hop, mabadiliko kwenye jamii yanayoambatana na Hip Hop, (bila kusahau) Hip Hop kama kitambulisho cha Vijana wengi sasa hivi.

Kilichonifurahisha zaidi ni kwamba anajua wapi pa kuanzia (kwasababu mambo ya utafiti yanahitaji maujanja, na kujua wapi pa kuanzia hurahisisha kazi); ataanza kuongea na wasanii ili kujifunza kama wanafikiri wana nafasi yoyote kwenye jamii.

Mimi binafsi nina maswali mengi mno. Lakini sasa hivi nitamuuliza Fid Q maswali machache tu kwanza ili aanze kuumiza kichwa:

1. Marekani inajulikana kama ndio chimbuko la Hip Hop, lakini sasa hivi inaonekana kama Hip Hop inaanza 'kurudi' Afrika (Soma makala kuhusu hili suala hapa). Je, kuna sababu za msingi au ni jambo la kawaida tu?

2. Wasanii wanajua maana ya Hip Hop? Wanaitumia ipasavyo?

3. Niliona filamu moja (documentary) inayozungumzia kufanana kwa maneno ya mitaani kutoka Marekani na Afrika Mashariki (ingawa lugha zitumiwazo ni tofauti). Kuna ukweli wowote ule?

4. Vipi kuhusu mambo yanayozungumzwa kwenye nyimbo mbalimbali. Sehemu mtu anapotoka (msanii) ina athari kubwa sana au ndogo kwenye nyimbo anazoimba? Au hutegemea zaidi mambo fulani mtu aliyopitia kwenye maisha yake binafsi? Ni sahihi kulundika wasanii kutoka Mwanza, Arusha au Dar kwenye kundi moja? Au tuangalie hadi vitongoji wanavyotoka?

5. Kuna baadhi ya wasanii kutoka Tanzania ambao wanaheshimika sana nje ya nchi ilihali bado wanatumia lugha ya Kiswahili kwenye nyimbo zao. Hii inakuwaje? Wengine wanatumia maneno kutoka Temeke!

6. Mabadiliko yanayotokea kwenye Hip Hop yanaakisi yanayotokea kwenye jamii? Au jamii huakisi mambo yanaongelewa na wasanii?

Nitaishia hapa kwa leo.

Ila kama una maswali zaidi au una maujanja yatakayoweza kumrahisishia utafiti huu, unaweza ukamtumia Fid Q barua pepe: cheusidawa (at) gmail (dot) com. Au unaweza ukatembelea blog yake (ina mipini yake karibia yote; cheki upande wa kulia).

Fid Q, Vijana FM inakutakia kila la kheri! Binafsi, nina uhakika kazi yako itawanufaisha wengi.

Makala nyingine kuhusu Fid Q zinapatikana hapa na hapa...

Budget 2010/2011

The size of the word reflects how often it was used in the 2010/2011 budget speech (wordle.net)

a 74 page document
79 - number of times the words "misaada" or "mikopo" appears
11,609,557 - amount in T.Shs of the budget
14% - basal income tax
20,277,100 - amount in USD set for research and development
628,591,000 - amount in USD set for Agricultural projects
2 Billion USD set for education expenditures
1 Billion USD set for health care
30% of total budget from donor sources
0% on import duty for transport buses (Fast Truck Project)..........


Hon. M. Mkullo, minister of finance (picture michuzi blog)

Click here for the full budget
How does the budget affect you?

Monday, June 14, 2010

Africa's Leaders of Tomorrow School (ALTS)

By BK

Everyday I read stories about the economic growth of China. I read about Germany's solutions, clean energy in particular, aimed at solving global challenges. I read about a student in a Tanzanian village who uses an oil lamp with a small floating wick, and that 60% of African population is living without electricity. I read that while two out of five Africans lack clean water supplies and Africa's economy is greatly reliant on international aid, the African population will double by 2030.

Some challenges are old. Some are new. I ask myself many questions. Some are: For countries to reaclh or maintain global leadership, should they focus on global solutions? Because global solutions are always also local while local solutions cannot always be global. If the correct answer is yes, then, is it the likeliest situation that an African country will never become a super power?

Obviously, we are living at a time when all agents of development, across all age ranges and professions, must work together to solve these challenges. Since life is only a choice that must have a purpose to be lived well; for Africa, I would propose a leadership school, Africa's Leaders of Tomorrow School (ALTS) that would involve young African students at the earliest time possible in solving African challenges.

ALTS would be a social business, and would place education at the service of the society. Interested mid-school students who are top in their classes, and who have demonstrated great leadership and risk taking skills in their communities would be admitted. They would be brought together and shown the greatest challenges that the continent faces in preparation for tomorrow's leadership. I am mindful that we learn best from the people who surround us. That's why guest speakers who are themselves entrepreneurs, policy makers, government leaders and infuential people would be invited to talk with the students.


The core subject, 'Africa and the World' would guide students through the history of Africa after independence, the challenges it faces and its e orts to solve them. An emphasis would be on why the continent is the poorest despite the great natural endowment it possesses. It would encourage debates and discussions, to emphasize on the development of leadership skills, entrepreneurial skills and global citizenship. It would be discussed on how leaders can play a greater role to improve the life of an African. The students will be required to write a project on a topic of their own choice but related to Africa and the World. An example of such a topic would be 'Africa, what is the missing link? a look at African governance.'

Not until we are aware of the challenges our small communities face, can we dream of solutions to national, continental or global problems. ALTS students would have to complete a minimum number of hours of community service in preparation for leading an interesting life in which serving others is the greatest character.

The major feature of ALTS curriculum would be to train young great minds to understand how every discipline has and can be used to solve the challenges humankind faces. I see this being met through talks by guest speakers and mandatory class discussions with course instructors.

I see graduates from the school become CEO's, politicians, activists, scientists, policy makers and economists of tomorrow, to mention but a few examples. ALTS students would become global citizens. They would not be fatalistics but able to embark on meaningful and unprecedented projects that would change the way Africa and the world operates. They would be able to integrate into the ever changing world in terms of technology, culture, science and politics while devising methods to integrate with solutions that aim at making Africa a bigger economy. With an emphasis on creativity, they would gain problem solving skills rather than mere knowledge accumulation. They would therefore be equipped with an ability to apply knowledge obtained in class to nd answers to the the problems of the society.

I would envision a family of such schools all over Africa under the social business concept that would prepare students to become leaders of tomorrow who would change Africa and the world at large.


BK, a guest columnist, is a senior at Jacobs University Bremen (in Germany) pursuing a B.Sc degree in Electrical Engineering and Computer Science. He hails from Mwanza, Tanzania.

Friday, June 11, 2010

Miaka minne iliyopita

Leo nimeamka alfajiri kabla hata jua halijachwea ili nifike mzigoni mapema; muda wa sherehe za Kombe la Dunia ukifika, niwe mbele ya runinga na glasi ya mvinyo nikiwashangilia watoto wa Bondeni wawapige bao Mariachi.

Miaka minne iliyopita nilikuwa sifuatilii vitu gani hasa vinavyotokea nyumbani, lakini nimekua na nimeanza kusoma vitu ambavyo vinanifungua macho. Na leo nimepata fursa ya kuperuzi bajeti yetu... Bahati mbaya bajeti yetu nd'o hivyo tena (bofya kwenye taswira):

Sio kama nimeshtuka saaaaana, ila kuna mambo mengi yanayoendelea ambayo yanatibua siku kama ya leo. Kama hicho kidogo tulichonacho, misaada na mikopo nchi yetu inayopata ingekuwa inatumiwa ipasavyo, sidhani kama ningekosa raha kiasi hiki.

Ni aibu kuendelea kuwapa madaraka watu ambao "labda" wanafanya mambo kwa manufaa yao. Tufanye nini? Ni kuwaondoa tu kwa nguvu ya hoja; nadhani kwa uchaguzi huu labda tume'shachelewa, kwahiyo tuanze kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa 2015? Ningependa kusikia mawazo yenu.

Nitaishia hapa na kuwaacha na maneno ya Jenerali Ulimwengu: Wawakilishi kama wafadhili, kosa!

Homa ya uchaguzi imepamba moto na wote wanaohusika kwa njia moja au nyingine wanachakarika. Wale wanaotarajia kujitokeza kama wagombea tayari wanapita huku na huku wakijitambulisha, na baadhi yao tayari wametangaza nia yao.

Miongoni mwa waliotangaza ni wale wale waliokuwa wabunge katika kipindi kinachomalizika hivi sasa, ambao wanatarajiwa wagombee tena, kwa sababu ni Waafrika wachache wanaokubali kujiuzulu kutoka katika nafasi za ‘uongozi’ ambazo mara nyingi ni nafasi za ulaji, ukwasi na utukufu. Nimesikia mara kwa mara watu wakishauri kwamba wabunge wasiruhusiwe kukaa bungeni kwa zaidi ya mihula miwili, lakini siamini kwamba siku moja Bunge letu litakuwa na busara ya kukubali ushauri kama huo.

* * *

... maana hii ya ubunge imevurugwa kabisa. Mbunge wa siku hizi anaangaliwa kama mfadhili, kama mtu wa “kuwaletea maendeleo” wananchi waliomchagua. Hiyo ndiyo lugha inayotumika: “Mkinichagua nitawaletea maendeleo.”

Dhana hii ambayo inamfanya mbunge kuonekana kama ‘mfadhili’ itatuumiza kwa muda mrefu, kwa sababu sioni ishara za kweli za kuifuta. Imekuwa ni njia moja rahisi kwa watu wasio na sifa za uwakilishi kujipatia ajira, nao wataiendeleza dhana hiyo kwa sababu inawafaa. Wananchi wenye sifa na uwezo mkubwa wa kuwa wawakilishi hawatafua dafu kwa sababu hawana uwezo wa ‘ufadhili’ huo.

* * *

Kila ninapoliangalia Bunge letu napata taswira ya mashaka. Bunge letu, kama ilivyo serikali yetu, lina taswira ya watoto wa wakulima na wafanyakazi, kama tulivyozoea kusema, hata kama leo tumeanza kusahau. Lakini kila miaka mitano inapoenguka, watoto wa wakulima na wafanyakazi wanazidi kupungua na watoto wa wafanyabiashara na wanamitaji wanaongezeka.

* * *

Lakini ongezeko la umasikini halitokani na wabunge kushindwa kufanya kazi yao. Ni kweli kwamba wako wabunge kadhaa ambao hata hiyo kazi ya uwakilishi imewashinda. Hawa ni wale waliokwenda kuomba kura miaka mitano iliyopita, wakachaguliwa na kisha wakahamia mijini na kuponda starehe bila kujali watu wao hata kwa kuwatembelea tu. Wakirudi kwao Oktoba ijayo watakiona cha mtema kuni.

* * *

Matokeo ya kura za mwezi Oktoba yatatupa mafundisho mengi, na hili linaweza likawa mojawapo ya mafundisho hayo. Ni matumaini yangu kwamba tutaweza kuyasoma vyema mafundisho hayo na kuyafanyia kazi kwa lengo la kuboresha miundo na michakato ya utawala wetu.

* * *

Kwanza kabisa, wananchi waelimishwe kuhusu maana halisi ya mbunge kama mwakilishi, kama mjumbe, na siyo kama mfadhili, na dhana hii ieleweke vyema kwa wananchi. Wanaposhiriki katika michakato ya uchaguzi wajue kwamba hao wanaowachagua si watu wa “kuwaletea maendeleo” kama wanavyowaangalia “wafadhili” bali ni wajumbe wao ambao jukumu lao kuu ni kuwawasilishia matatizo yao na hoja zao katika baraza la Taifa na huko ndiko upatikane ufumbuzi wa matatizo yao katika muktadha wa kutafuta utatizo wa matatizo ya nchi nzima kwa pamoja.

Tusiwaruhusu wabunge wetu kujifanya ni Papa Noeli, Father Christmas anayekuja na zawadi kwa kila mtoto, kwa sababu mbili kuu: kwanza katika dunia ya kweli hakuna Father Christmas; pili tunatakiwa tuache kuwa watoto.

Soma makala nzima hapa (bofya)...

Thursday, June 10, 2010

Utaenda 'jeshini'?

Wengi wetu tumesikia simulizi za kusisimua kutoka kwa wazazi wetu pindi walipokuwa jeshini (National Service). Nyingi zinahusu shida, uvumilivu, ufanisi na uzalendo. Ingawa kuna waliochukia maisha magumu waliyoyapata walipokuwa jeshini, wengi wao wanakumbuka kipindi hicho kwa tabasamu. Binafsi mama yangu anasikitika kuwa vijana wa leo hatupitii kimbembe kama alichopitia yeye baada ya form six kwa mwaka mmoja pale JKT Ruvu.


Mpango wa National Service ulianzishwa na Mwl. Nyerere katikati ya miaka ya 60 kwa nia ya kujenga taifa lenye watu wazalendo, jasiri, werevu na wakakamavu. Mchakato huu ulikuwa wa lazima kwa wanafunzi wote wanaomaliza shule ya sekondari kwenda katika kambi za jeshi na kupitia mafunzo mbalimbali ya kijeshi na kielimu kwa mwaka mmoja. Mpango huu ulifutwa mwaka 1992, na hivyo kufanywa wa hiari.

Nchini Tanzania, kuna mjadala umejitokeza kuhusu kurudishwa kwa mpango wa National Service kwa vijana wa sasa. Je, itakuwa vibaya tukirudisha mchakato huu kwa wanaomaliza sekondari kutumikia taifa kabla ya kujiunga na chuo au sekta binafsi? Simaanishi tuwe na national service ya kijeshi, la hasha, bali tuanzishe mpango kwa ajili ya wahitimu wa sekondari utakaoweza kuwapeleka vijana wetu vijijini kufundisha masomo kama hisabati, na lugha kwa kipindi cha miezi 6-12. Au hata kuwatumia vijana hawa katika hospitali zetu - kwenye awareness campaigns za ukimwi/malaria vijijini, au kuwatumia kwenye vituo vya kilimo, vituo vya wazee/walemavu/watoto yatima na hata kwenye mabenki. Ilimradi tu mchakato huu usiwe wa kitumwa, au mateso bali uliojaa elimu mbadala wa vitendo ili kujenga taifa imara.

Wednesday, June 9, 2010

Did you guys see this?

Just saw this on Lin The Fin's Blog (Posted on the 17th May, 2010; I don't understand how I missed the whole saga... I guess the officials did their best to keep things quiet.):

Last week presidents Jakaya Kikwete and Armando Guebuza inaugurated the long-awaited Unity Bridge that spans 720 meters over the river Ruvuma between Tanzania and Mozambique. The two countries are finally connected!

Except they are not.

During the project of spending 34 billion Tanzanian shillings ($ 24 million) nobody thought to build customs posts or roads to the bridge. It's 165 km from the bridge to the nearest paved road in Mozambique, and 56 km to the paved roads in Tanzania. The nearest towns are Mocimboa da Praia (275 km) and Lindi (240 km).

These people built a bridge linked to nothing. It can't have been built so suddenly that it took the Ministry of Planning by surprise. It can't have been so low-profile that nobody noticed that it was happening. According to the Controller and Auditor General (report on financial year 2008/2009) the bridge is "useless".

Finance minister Mustafa Mkulo says "It was unfortunate that there wasn't adequate coordination when the project was being implemented".

No, it's not April fools' day!

Iba kura, uwatishe, ukishindwa kubali

Hayo sio maneno yangu, jamani! Ni kichwa cha habari cha mtiririko wa makala za Jenerali Ulimwengu kwenye gazeti la Raia Mwema.

Nafahamu fika kuwa Vijana wengi hatupendi kufuatilia Siasa, hatuna mpango wa kupiga kura na hatufanyi mambo muhimu yanayohusiana na upatikanaji wa viongozi kwenye nchi zetu. Lakini, unadhani tutapata suluhisho la haya matatizo yetu kwa kunung'unika tu? Kupiga kelele kwenye forums?

Leo sina mengi sana kuhusu hili jambo, lakini napenda kuwaasa tufumbue macho na tujaribu kubadili fikra zetu. Tuitikie mwito pale jamii inapotuhitaji -- kuna matatizo mengi kila kona kama mnavyojua na ni jukumu letu kujitosa na kujaribu kuyatatua.

Nakusihi ufuatilie makala za Jenerali ulimwengu ambazo zinazungumzia uchaguzi ujao -- kuna mengi sana ya kujifunza.

Maneno ya Jenerali:

KATIKA makala zangu zilizopita nimekuwa nikijadili masuala yanayohusiana na uchaguzi mkuu ujao na jinsi tunavyojiandaa kukabiliana nao. Miongoni mwa mambo mengi ambayo nimejaribu kuyajadili nimekuwa nikisema kwamba sisi Waafrika bado hatujejenga uelewa wa kutosha wa kujua ni nini maana ya uchaguzi.

Bado tunaenenda, hasa tukiwa madarakani au tukiwashabikia walio madarakani, kama vile uchaguzi ni kitu kibaya ambacho hata hivyo hatuna budi kukivumilia kwa sababu, kutokana na sababu zisizozuilika, hakiepukiki. Hii ni sawa na kung’oa jino lililooza.

Ndivyo ilivyo katika nchi zote za Kiafrika. Uchaguzi ni jambo tunalokubali kuliingia shingo upande kwa sababu hivi sasa, katika dunia ya leo, hatutaeleweka duniani kote, na hasa kwa “wafadhili” ambao wanatuambia hatuna budi kuonyesha kwamba tunajali misingi fulani ya demokrasia.

Kama Waafrika, tunachoogopa hasa ni hatari ya kukosa misaada iwapo tutaonekana kama hatutaki kufanya uchaguzi. Tutanyimwa misaada, na kisha tutazomewa kila tuendako Ulimwenguni. Tutaonekana kuwa watu wa ovyo, watu wa zamani mno, watu wasio ‘poa.’

Kama isingekuwa mambo hayo mawili, naamini kwamba watawala wetu wangekuwa wamekwisha kutafuta lugha laini ya kutueleza kwamba uchaguzi ni jambo la hatari lililoletwa na wageni kwa lengo la kutuzuga na kutudumaza kwa kutufanya tuzame katika malumbano yasiyoisha ya kisiasa na tusahau mambo muhimu yanayohusu maendeleo yetu… kama kilimo.

Labda, wangeweza kuogopa kwamba wanasiasa wenzao katika upinzani wasingeikubali lugha hiyo na mantiki hiyo na wangeziingiza nchi katika migomo isiyoisha na ingewezekana hata kukatokea maasi kutokana na wananchi kuchoshwa na kundi linalong’ang’nia kuwa madarakani kwa kutumia kila hila ingawa ni dhahiri kwamba limeshindwa kufanya kazi ya kuwaletea maisha bora wananchi wao.

Endelea kusoma hapa...

Tuesday, June 8, 2010

Zum zum zum...

Lyrics:

Zum zum zum,
Eeeeh mama nyuki lia we.


Zum zum zum,
Eeeeh mama nyuki lia we.

Toka mbali, kutafuta, ua zuri, la maua,
Zum zum zum,
Eeeeh mama nyuki lia we.



Haya, wenzangu mnakumbuka nyimbo gani? Maana'ke mkiniachia mwenyewe niendelee, blog nzima itajaa:

Mabata madogo dogo, yanaogeleeaa!
Katika shamba zuri la bustani!
Yanapenda kulia,
kwaa kwaa kwaaa kwaaaa kwaaa kwaaa!...

Utu uzima dawa, jamani. Kama ingewezekana kurudi utotoni...

Shukrani kwa da' Subi (sio kwa nyimbo! - bali kwa kutuonesha wapi pa kuzipata videos kutoka Bongo).

Watanzania na Ujio wa Brazil



Kipyenga cha mwisho kimelia, huku Brazil wakishinda mpambano dhidi ya Taifa Stars kwa magoli matano kwa moja. Mazungumzo na mabishano juu ya mechi hii iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na Watanzania wengi itabaki kuwa gumzo la jiji kama sio nchi, kwa wiki kadhaa zijazo. Watanzania tutaelekeza nguvu zetu kwenye kupiga domo juu ya mechi hii huko vijiweni kabla ya hali halisi ya maisha yetu duni kutuzindua kwenye starehe hii iliyo dumu kwa dakika 90.

Ujio wa Brazil umepokelewa kwa hisia tofauti, wengi wakishabikia kuwa hatimaye watamwona mchezaji mahiri wa Brazil, KaKa kwa macho yao wenyewe. Kuna kundi dogo la watu waliotaka Watanzania tususie mechi kwani haina manufaa yoyote katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu. Zogo hili la ujio wa Brazil lilianza kupaa kwa kasi pale Bw Paulo Kamau wa Kenya alipobeza uamuzi huu wa Tanzania kuwalipa fedha nyingi vijana hao wa Samba.

Tanzania Football Federation (TFF) wamekuwa kimya kuzungumzia kiwango halisi walichowapa Brazil, wakati mwazoni walidai kuwa Serikali iliwatengea fungu la dola za Kimarekani milioni sita. Tovuti ya BBC wamedai kuwa TFF iliwalipa dola milioni mbili na nusu. Kiasi taslimu cha fedha walicholipwa Brazil bado kinabaki kuwa tata, huku Raisi wa TFF ndugu Leodegar Tenga akidai kuwa, "It's definitely that the coming of top players in the world will be a big boost to local football as well as the tourism sector,".

TFF imejitetea kuwa, ujio wa Brazil utachochea maendeleo katika soka na kwenye sekta ya utalii. Hizi ndizo sababu kuu mbili zakutetea matumizi makubwa ya fedha ya kuwalipa Brazil kuja kucheza na Taifa Stars, sasa swali ni hili, Je Tenga na TFF wana hoja ya msingi?

Mimi binafsi sidhani kama hoja hiyo ina nguvu ya kutosha kuhalalisha matumizi ya hivyo vijisenti walivyowalipa Brazil, na hoja zangu ni kama ifuatavyo. Soka la Tanzania limekuwa kichwa cha mwendawazimu kwa miaka mingi, na mimi nina uhakika wengi tunajua ni nini kinatakiwa kufanyika ili kuinua soka la Tanzania. Tatizo la kwanza, tunapenda kukimbia kabla hatujajua kutembea, na hoja hii aliizungumzia kocha wa Taifa Stars wa sasa ndugu Marcio Maximo alipotoa ushauri wake juu ya soka la Bongo. Mimi sio mtaalamu saana wa soka wala sijawahi kuwa kwenye kamati ya ufundi wa tunguli, lakini hoja ya Maximo itaungwa mkono na wengi wenye uwerevu. Watanzania inatubidi tuanze kujenga utamaduni wa kusikiliza wataalamu na sio wanasiasa wasio jua lolote.

Sasa tukija kwenye sababu ya pili, ya kuwa ujio wa Brazil utasaidia soko la utalii, nadhani kuna mambo kadhaa ya kuangalia kwa utaratibu. Jambo la kwanza, tuna uhakika gani ujio wao utaongeza ujio wa watalii? Najua moja ya jibu la swali hili litakuwa, kwasababu mechi inaonyeshwa moja moja katika nchi zisizopungua mia 160. Hii inaweza saidia; lakini wasiwasi wangu ni kuwa, kuna utafiti mdogo umefanywa katika kuhakikisha kuwa hii ndio njia bora ya kutangaza nchi yetu. Katika mpango huo, je tuliangalia njia mbadala ambazo zingetugharimu fedha kidogo zaidi na ambazo tungekuwa na uhakika zaidi kuwa zitazaa matunda?

Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Shamsa Selengai Mwangunga (MB) alipotoa makadirio ya Wizara yake Bungeni, aliongelea mipango kadhaa ya Wizara yake. Moja ya mipango hiyo ilikuwa ni kuongeza utalii wa ndani, kwa kuwapunguzia Watanzania viingilio katika mbuga za wanyama na sehemu nyingine za kitalii. Mkakati huo ni mzuri, lakini bado tunategemea zaidi watalii wa nje. Lakini kidogo kimefanyika kuhamasisha watalii wa nje kuja nchini. Tanzania bado inatajwa kama nchi yenye viwango vikubwa (fees) kwa watalii, ukilinganisha na Kenya na Uganda. Kenya na Uganda walipunguza viwango vyao baada ya uchumi wa dunia kuyumba, lakini Tanzania bado tumeacha viwango vikiwa juu. Sasa hapo ndio kuna mgongano wa mawazo -- huku tunatumia mamilioni kadhaa kutangaza nchi, lakini hatupunguzi viwango. Hao watalii wataishia kwenda Kenya na Uganda na kukwepa Tanzania, hivyo mwisho wa siku tunajaza maji kwenye pekecha.

Ripoti ya Repoa iliyokuwa inazungumzia The Role of Tourism in Poverty Alleviation in Tanzania ni ripoti inayotoa mapendekezo yakinifu. Pamoja na ripoti hiyo iliyotoka miaka saba iliyopita, lakini mapendekezo yake bado yana umuhimu, sasa sijui mapendekezo mangapi ya ripoti hiyo yalifanyiwa kazi na Serikali kupitia Wizara yake husika. Mimi nakubali sekta ya utalii inaumuhimu mkubwa, hasa katika kuchangia kupunguza umasikini. Lakini je, tumeboresha sekta hiyo kwa kiasi gani? Tanzania leo tunaweza kusema huduma zetu za utalii zinaweza kushindana na nchi nyingine za Afrika au bado huduma zetu ni duni. Miundombinu bado ni tatizo kubwa, lakini tumeng’ang’ania kutangaza nchi. Jamani, akili ya namna hii haina tofauti na akili ya mtu anayekaribisha wageni kabla ya kufagia nyumba na kuhakikisha kila kitu kiko sawa.

Timu ya Brazil nd’o hiyo imekuja na kuondoka, sasa ningependa kuona kama malengo ya mpango huo yatafikiwa; soka ya bongo kuhamasika na hao watalii kuongezeka. Mimi kwa kiasi fulani ninakubaliana na baadhi ya watu waliotaka Watanzania tususie mechi hiyo na pia ninakubaliana kwa kiasi fulani na mawazo ya Kamau. Tanzania ni nchi masikini kutumbua fedha zote hizo kwenye kitu ambacho hatuna uhakika kitalipa. Tanzania tukiwa kama nchi moja masikini sana duniani, lazima tuwekeze fedha za walalahoi kwenye mambo ya msingi zaidi, sio kwenye starehe za dakika mbili tatu. Majuzi tu, tulikuwa wenyeji wa mkutano wa uchumi wa dunia. Ukiniuliza mimi hiyo ilikuwa nafasi nzuri kutangaza nchi. Je, tulifanya hivyo ipasavyo, au tulishangalia tu wageni waliokuja?

Aliyesema ng’ombe wa masikini hazai, hakukosea. Na msemo huu ni kweli kwani, ni watu masikini ambao mara nyingi hufanya maamuzi ya papara bila kufikiria kuwa kuna kesho. Tuendelee kuzungumzia ni jinsi gani Brazil walivyopigwa chenga na Taifa Stars, lakini wao haoooo wanaelekea kwenye Kombe la Dunia, Sisi je? Kamau alivyozungumzia “character” yetu Watanzania hakukosea sana. Pamoja simuungi mkono na kejeli zake, lakini alikuwa na hoja. Hivi kweli watu wazima tunaweza kusema,” tumefungwa lakini tuliwapiga chenga”. Hilo ni jambo la kushabikia kweli? Tukiendelea na akili hizo sisi kila siku tutanyonywa na kukandamizwa kwani tumekuwa watu wa kufurahia mafanikio madogo, tena ya kijinga, badala ya kusimama na kupigania maendeleo makubwa yenye maana. Tumezidi kuwa wa ndio mzee, badala ya kuuliza maswali, kupigania haki zetu na kupigani uwajibishwaji wa viongozi wabovu wenye kunuka ufisadi. Watanzania, hivi ndio tumekubali kuwa umasikini ni utamaduni wetu?

Watanzania wenzangu waliojitutumua na kulipa viwango vikubwa kuwaona Brazil, je, ulifikiria mechi hiyo kama ina manufaa kwa nchi yetu. Hivi ni wewe huyo huyo unayelalamika kuwa barabara zimechakaa na msongamano wa magari umekithiri. Wewe ulilipa kwenda kumwangalia KaKa, je nyumbani kwako haupatagi matatizo ya kukatiwa maji na umeme mara kwa mara au unajenerata na bwana la maji nyumbani? Leo hii ukalipe fedha zote hizo kuwaona Brazil, alafu kesho unafanya kila uwezalo kukwepa kulipa kodi na kupokea rushwa. Watanzania tunazungumzia sana kuhusu tulivyo masikini, lakini hapo hapo tunataka starehe zinazotushinda uwezo. Naona tunataka kulazimisha maji yachanganyike na mafuta; kweli Tanzania tuna akili zinazotutosha sisi wenyewe.

Ushauri wangu ni huu, kama tulivyopigania tiketi za kumwona KaKa, basi moyo huo huo wa kupigana usiishie hapo. Moyo huo uendelee katika kupigania maendeleo, kupinga viongozi wabovu, tuwe na kiu ya maendeleo na ari ya kuchapa kazi kama tulivyoshangilia magoli ya Brazil kwa nguvu zetu zote. Tuache kuendeshwa na hisia bali tuendeshwe na fikra, kwani ujio wa timu ya Brazil hauwiani na msemo wa ‘mgeni njoo wenyeji tupone’, bali ni ‘mgeni njoo wenyeji tuzidi kuumia’. Mimi ninawatakia kila la kheri Brazil kwenye kombe la dunia na sisi kama kawaida yetu tutaishia kulishangalia kwenye runinga, kama utamaduni wetu, kwani sisi ni nambali moja kwa kushangalia maendeleo ya wengine na kuiga mambo yasiyo na manufaa.

Picha kwa hisani ya cartoonist Gado

Monday, June 7, 2010

Kama chenga tu, tumewala

Tanzania 1 - 5 Brazil (Highlights)



Leo tufurahie chenga za Ngassa na goli la Aziz. Kesho tunaanza kuuliza maswali -- vipi ilikuwaje uwanja haukujaa? Hela za kuwalipa zilipatikana wapi? Faida n.k.

Mimi na blogs na facebook!

Na "Mtu Fulani"

Kama kawaida yangu, napata habari sahihi kutoka kwenye tovuti yangu ya Wavuti huku nikipiga mzigo. Nikipata upenyo natupia jicho blog ya Michuzi Jr kucheki ana picha gani asubuhi hii. Ni mwiko kuvunja utamaduni wa Mtanzania mwenye mtandao -- lazima nicheki mambo gani yanajiri kwa Michuzi aka Mzee wa Masafa ya Mbali. Ah! Hakuna atiko mpya ya Mashaka na inaonekana kama pamedoda kiasi fulani. Ninaperuzi kuelekea chini taratibu nikiangalia picha za matukio mbalimbali; nakutana na post ya salamu kutoka kwa Kamau!

Mhh! Kuna maoni zaidi ya 150?? Mashaka kabadili jina nini!? Nasoma ujumbe wa Kamau taratibu halafu najitosa kwenye maoni. Wabongo kumbe tuna hasira kiasi hiki? Wachafuzi wa hali ya hewa ni wengi, lakini kama wahenga walivyosema, penye wengi hapaharibiki neno. Naona baadhi ya maoni yenye mawazo mazuri. Lakini hizi nguvu zingepelekwa kwenye matatizo ya nchi zetu hizi mbili nadhani tungepiga hata hatua moja ndogo ya mtoto mdogo.

Baada ya kumaliza kazi zilizoko mbele yangu, naenda facebook kuona masela wanafanya nini na kutembelea kurasa za maselebriti wa Bongo. Namcheki msela wangu kutoka kitaani, Gillsant -- mshkaji hata akiweka nukta kwenye status yake, comments zinatiririka! Ana marafiki karibia buku tano... Kwahiyo wale wenye blogs zinazotafuta umaarufu hutumia ukuta wake kama ubao wa matangazo.

Namcheki Prof. Jay ambaye alipotea kidogo baada ya kuonekana kavaa uzi wa kijani. Kama kawaida yake anabadilishana mawazo na mashabiki wake. Inaonekana muda na ukimya vimepoza maswali yaliyokuwa kwenye vichwa vya wengi. Naenda kwenye ukurasa wa Fid Q kuangalia kama ameposti mistari na vina vipya. Jamaa mistari yake imeshiba; shule tosha na anaweza kukuambukiza uanaharakati kutokana na msimamo wake.

Ngoja ni-search kucheki kama Juma Nature naye yumo facebook. Kudadadadadeki, Nature ndani ya nyuuumba! Ana mashabiki 46 -- ngoja tucheki itamchukua muda gani kufika mashabiki 1000.

Dah! Nadhani inatosha, ngoja nirudi mzigoni. Lakini kabla ya ku-sign out lazima nipate ile kitu roho inapenda: Picha murua.

Nabofya sehemu fulani na naishia kwenye ukurasa wa Vijana FM. Dah, panatia huruma kwasababu pamedoda ile kinoma. Labda wakiweka picha nzuri za watu maarufu watapata mashabiki zaidi (angalau wafike 500 tu).

Nachoropoka kutoka Vijana FM na kuishia kwenye ukurasa wa Ray C. Naperuzi picha zake haraka haraka kwasababu nimeshaziona nyingi.

Vitu vitamu havihitaji haraka kwahiyo natembelea ukurasa wa K-Lynn mwishoni kabisa. Mke wa mtu hasifiwi, lakini nimeamini kuwa Wabongo ni wabishi!

Na-sign out na kutupia jicho blog ya Mange. Duh, nilidhani blog bado ni changa lakini inapata hits zaidi ya buku tano kwa siku! Kwa mwendo huu, hii nd'o itakuwa mama ya blogs zote Bongo. Michuzi itabidi akae chonjo.

Ngoja nirudi mzigoni.

UNAWE-Tanzania

Kuna baadhi ya mambo unayaona au kuyasikia na hukupa motisha ya aina fulani - hasa yanapotokea nyumbani. Kitu muhimu zaidi ambacho hukufanya hata uanze kujivunia ni watu wanaojitolea kuwafundisha wadogo zetu na kuwaandaa na dunia hii ambayo inaendelea kutekwa na sayansi ya teknolojia.

Mara nyingi nikitembelea tovuti ya UNAWE-Tanzania, nashindwa kujizuia kujiuliza maswali mengi. Ingekuwa vipi kama ningefundishwa na timu ya kaka Mponda? Je, kama ningeoneshwa mwezi, sayari nyingine, nyota na vimondo wakati bado niko mdogo, mambo yangekuwa tofauti? Kusema ukweli kuna wakati nawaonea donge watoto wanaopewa nafasi na UNAWE-Tanzania. Na nina uhakika juhudi zao zitazaa matunda ambayo yataleta mabadiliko kwenye jamii yetu kwa namna moja au nyingine.

Nakumbuka nilikuwa napenda sana masomo ya sayansi. Na nilijifunza jinsi ya kukokotoa maswali ya lenzi (i.e. ray optics), nilikariri majina ya sayari zote (na idadi ya miezi yao) na hata umbali wao kutoka kwenye jua. Lakini nilikuja kuiona telescope kwa mara ya kwanza nilipokuwa kidato cha pili! Nadhani unaelewa kwanini nawaonea donge wadogo zangu.

Wiki chache zilizopita, UNAWE-Tanzania walipokea vitabu, CDs na vifaa vingine muhimu vya kufundishia. Bahati mbaya au nzuri, kuna baadhi ya vitabu ambavyo itakuwa vema vikitafsiriwa kwenye lugha ya Kiswahili. Kwahiyo, wasiliana nao kama unaweza kuwasadia.

Nakusihi utembelee tovuti yao mara kwa mara ili kufuatilia vitu wanavyofanya. Kama hutaweza kuwasaidia kwenye mradi huu wa kutafsiri vitabu, nina uhakika hapo baadae unaweza ukawasaidia kwa njia nyingine.

Pongezi zangu ziwaendee UNAWE-Tanzania! Nitaendelea kuwatupia jicho kama kawaida yangu.

Sunday, June 6, 2010

Mzungu Kichaa anena na Shurufu

Mara ya kwanza nilipoona video ya wimbo Jitolee wa Mzungu Kichaa, nadhani niliicheza zaidi ya mara kumi mfululizo! Sehemu ambayo mpaka leo bado inanipa tabasamu ni pale jamaa anapowarusha masela Kariakoo (muda 0:55):



Halafu, hapo bado sijaanza kuongelea jinsi gitaa lilivyokung'utwa ile kisawasawa -- amelitekenya kama Diblo Dibala!

Kichaa ana hadithi nyingi mno ambazo nina uhakika watu wengi watapenda kuzisikia. Wiki iliyopita Shurufu aliongea na Mzungu Kichaa kwa kirefu na mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo (ung'eng'e au ngeli itahitajika):

“I became Mzungu Kichaa not too long ago; when I released my [debut] album 'Tuko Pamoja' in May 2009. So, in that sense I am new to the game as an artist, under the name Mzungu Kichaa. But in reality, I have been around and I’ve been involved in Music ever since I was…very small. And also I have been involved in Bongo Flava since the start of Bongo Flava, recording at Bongo Records. I went to IST with P-Funk aka Majani…just before he got expelled for stealing the school’s musical equipment so he could produce [laughs].

“... I did stuff behind the scenes like on Juma Nature's [2001] album 'Nini Chanzo' and then I did this song which featured quite significantly on Solo Thang's album, ‘Mambo ya Pwani’ which was a big hit. My role was quite significant cause I actually helped…program it, pretty much all of it, cause the remix took my guitar as the foundation of the program. So we did that and that’s kind of what made me known within the industry but I wasn’t known by the public. The name [Mzungu Kichaa] I got…at Bongo Records [given to me] by Juma Nature way back then when I was working there. So I decided to take up the name...

Endelea kusoma hapa...

Saturday, June 5, 2010

Tovuti ya Wahapahapa Na Sanaa..



Leo hii sanaa bado haijapewa heshima na kipaumbele kama inavyotakiwa, pamoja na sanaa kuwa kioo cha jamii. Tovuti na blog zimeanza kumea kama uyoga, lakini chache zimekuwa zikitetea nafasi ya sanaa katika jamii na haki na umuhimu wa wasanii ndani ya jamii.

Wahapahapa ni moja ya tovuti ninazoweza kusema zimejikita katika sanaa, siyo kuishia kuzungumzia sanaa tu. Kitu kilichonifurahisha na tovuti ya wahapahapa, ni kuwa wameweka michezo ya kuigiza ya redio katika tovuti yao. Hii inawapa fursa hata walio mbali kufaidi sanaa hii kongwe iliyopewa kisogo kutokana na ukuaji wa utandawazi. Nadhani kizazi cha enzi zile tunaweza kukumbuka ile michezo ya akina marehemu Pwagu na Pwaguzi katika redio ya Taifa, RTD.

Tembelea tovuti hii ya Wahapahapa na sikiliza michezo hiyo ya kuigiza na pia kujisomea mambo mengi mengineo ya kuelimisha kupitia sanaa.

Antivirus Mixtape iko jikoni…

Msanii mkongwe Sugu au kama alivyokuwa akifahamika enzi zile kama Mr II anakuja na album itakayoitwa antivurus. Mixtape hii itakayoshirikisha wasanii wengi wa bongo flava, inakuja kwa dhumuni la kupigania sanaa hii na kupigania haki ya badhii ya wasanii wa sanaa hii ya bongo flava na bongo hip hop.



Hivi karibuni kumekuwa na mijadala kadhaa kuhusu mwelekeo wa sanaa ya bongo flava, lakini kidogo kimekuwa kikifanyika kuitetea ipasavyo. Katika makala ya penye kufuka moshi niliweza kujadili uhasama unaoanza kujengeka kati ya wasanii wapya na wale wakongwe. Wasanii wakongwe wamekuwa wakiwalaumu wasanii chipukizi kuwa wanachangia katika kuudhofisha mziki huu wa bongo flava. Nadhani kila mtu analake la kusema juu ya malumbano haya, kutegemeana na upande unaoshabikia.

Shauku yangu na hii mixtape ya antivirus ya Sugu ni kuwa itasaidia kuweka hili tatizo bayana kwa kuwataja wahujumu wakuu wa sanaa hii. Nadhani muda umefika kwa baadhi ya wasanii kuweka msimamo na kusimama pamoja kutetea mziki huu. Tuombe harakati hizi ziweza kuzaa matunda, kwani wengi wanaamini mziki huu umepoteza dira kwa kiasi fulani, sasa sijui kama wewe unakubaliana au kupingana na hoja hii.

Habari hii kwa hisani ya bongo5.com

Friday, June 4, 2010

Mimba

na Lars Johansson (with English subtittles)

Kama mjuavyo, idadi ya vifo vya watoto wachanga nyumbani kwetu ni kubwa mno. Filamu hii inajaribu kuchunguza sababu za haya matukio -- kutoka wilaya za Lushoto, Moshi na Serengeti.


Love in the time of Aids

Na Lars Johansson (with English subtittles)

Hii ni hadithi kutoka kwenye kambi ya wakimbizi Kanembwa, Tanzania. Katika filamu hii, Noe Sebisaba anaeleza jinsi alivyojitokeza na kuuambia umma kuwa ana Virusi vya Ukimwi.


11 minutes on Poverty

by Lars Johansson (with English subtittles)

Video clips from six Maweni Farm documentaries from Tanzania, Kenya and Nigeria, prepared for Sida (2008).