Friday, June 4, 2010

Uwanja wa Fisi

Na Lars Johansson (with English subtittles)

Kifuatacho ni kisa cha dada Elisa kutoka Uwanja wa Fisi. Nadhani wengi wetu tumeshaiona hii filamu, lakini nimeona sio vibaya nikiipost tena hapa kwa ajili ya wachache ambao hawajawahi kuiona.



Pia, timu ya Lars imetengeneza filamu nyingine kama hizi nyingi tu ambazo zinajadili matatizo mbalimbali -- kuhusu umaskini, vifo vya watoto wachanga, matatizo yanayowakabili wavuvi wa Ziwa Viktoria n.k. Tutazipost documentaries zote hapa.

Uzuri wa filamu hizi ni kwamba Lars (na wahusika wengine) wanaenda sehemu husika na wanawaacha wananchi watuambie hadithi zao kama zilivyo. Hii ni tofauti na watengenezaji wa filamu kama hizi ambao wanajaribu 'kupindisha' ukweli ili kujaribu kuwasilisha ujumbe wanaotaka.

Ili kurahisisha jinsi ya kuzitafuta hizi filamu hapa Vijana FM, filamu za aina hii (zilizotengenezwa na Lars) nimeziongezea label ya "LARS". Kwahiyo cha kufanya ni kubofya neno "Lars" tu kwenye orodha ya categories iliyopo kulia.

Hadithi fupi

Kwa wale ambao walikuwa wanafuatilia hadithi fupi hapa Vijana FM (unaweza ukazipata hadithi za awali hapa), nataka kuwataarifu kuwa zoezi la kuzipost hapa litasitishwa kwa muda. Huu uamuzi unatokana na ushauri niliopewa na baadhi ya wasomaji, ndugu, jamaa na marafiki kwa kuwa naangalia kama kuna uwezo wa kuzikusanya na kutoa kitabu hapo baadae (kama nikipata nafasi hiyo).

Kitabu (kitaitwa "Kelele za Ukimya - kutoka Uswazi") kikikamilika nitawataarifu na nitapost baadhi ya hadithi hapa . Wakati huo huo naelewa kuwa wahusika wanaweza wakakataa kuchapisha kutokana na mambo ninayoongelea na sababu nyingine wa kadha. Lolote litakalotokea, utapata fursa ya kuzisoma -- iwe kutoka kwenye kitabu, hapa Vijana FM, forums n.k.

Nawatakia siku na kazi njema!

__

SN.

Thursday, June 3, 2010

Unakumbuka enzi zile?

Kucheza gololi, matairi, magari ya makopo, cha ndimu (angaisha bwege, tobo bao na gombania goli), kutengeneza manati na kuwinda ndege, kudaka panzi, kidali po, kombolela... Bila kusahau kufuga samaki (nilikuwa na magapi kibwena! i.e. guppy aka Poecilia reticulata).


I got this film from Jadili Africa facebook page. Jadili Africa was founded in 2010 by conscious Africans who always dream of a peaceful Africa that is in peace with itself. I will encourage you to join the group if you want to see more short clips, articles, documentaries and news about Africa -- covering all sorts of angles; from politics to sports, cultures to myths, history to tourisms, shaky times to triumphs and many more.

Tamasha la Kibera

Jumapili iliyopita lile tamasha la kuhamasisha Vijana wa Kenya (hasa wa Kibera, Nairobi) kufuatilia mabadiliko ya katiba lilifanyika. Na ifuatayo ni taarifa kutoka NTVKenya:



Napenda kuwapongeza waandaji na wasanii waliojitolea kutumbuiza kwenye tamasha. Ni mfano wa kuigwa.

Tuesday, June 1, 2010

Technology transforms Tanzania



I am glad that, technology is picking up the pace in helping farmers, for example to find potential buyers/ markets for their produce, more easily & efficiently. This is promising, that the government is starting to take agriculture more serious. I have always find it interesting, if not ironic, that Tanzania is called the country of farmers (because many people still relay on agriculture)but the agricultural sector is given the least attention & priority.

There is a lot of work to be done still, for example; improving technology in cultivating the land. Many farmers still use hand hoes, instead of tractors, something that limits how much food is harvested annually. Secondly, Irrigation systems need to be put in place, because depending on the rains that are not always reliable, will be inviting hunger every year. However, this is a good step, because as they say, every long journey starts with one step at a time.

Waafrika tuna asili moja?

Na VR

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiumia roho mno kwa jinsi watu kutoka Afrika tunavyolundikwa kwenye kundi moja kiasilia. Kukiwa na tatizo utasikia, waache hao, ni tabia ya Waafrika hio, hawatakoma. Bara/nchi yao imelaaniwa.

Ukweli ni kwamba bara letu lina watu wenye asili na tofauti nyingi mno kimaumbile, kiutamaduni na hata ukiingia kwenye chembe chembe za DNA. Ukiangalia bara la Ulaya, Wajerumani wamepakana na Wafaransa, lakini watu hawa hawapendi kabisa kufananishwa. Ukienda Amerika ya Kusini, ni mwiko kumuita mtu anayetoka Colombia Mbrazili.

Utafiti unaonesha kwamba idadi kubwa ya watu wenye asili ya Afrika wana maumbile mengi na tofauti kuliko watu katika mabara mengine -- hasa ukiangalia chembe chembe L1, L2 na L3 mtDNA (Krings et al, 1999).

Wanahistoria waliojaribu kutafuta jinsi ya kuelezea asili ya Mwafrika, walifanikiwa kusambaza mawazo yao pande zote za dunia. Mengi ya mawazo hayo yawezekana yalikuwa ya kudhani tu au imani. Inasemekana kuwa asili ya Mbantu ni misitu ya Kongo. Ingawa yawezekana ikawa ni kweli, nina hofu ikawa ni imani ya wenyeji wa pale waliodhani kuwa wako katikati ya dunia. Na mtafiti aliyefika pale hakuweza kupata mawazo ya staarabu, makundi au falme nyingine zilizokuwa mbali na eneo utafiti huo ulipofanyika.

Kwahiyo elimu iliyopatikana hapo haikuwa ya kutosha au tuseme ilikuwa hafifu. Ingawa mtafiti huyo alilifahamu hilo, aliamua kufanya hitimisho kuwa Wabantu wote walitokea eneo lile. Ninaweza nikahisi kuwa, Kibantu asili kama ilivyokuwa Kilatini na sasa Kiingereza, ilikuwa lugha ya wasomi wa kale hapa Afrika. Sasa, idadi ya watu wenye asili tofauti ilivyokuwa inaongezeka, lugha nayo ilikua na kubadilika taratibu ingawa iliendelea kuwa na asili yake miaka nenda rudi. Hitimisho hili halina uhakiki kuwa asili ya Wabantu na hasa watu wa kusini mwa jangwa la Sahara wawe na asili ya misitu ya Kongo. Cha kushangaza, chembe L0 mtDNA inayosemekana kuwa mzazi wa L1, L2 na L3 mtDNA, inahisiwa kuwa na chanzo chake Afrika Mashariki.

Kwanini Waafrika tukubali kuwekwa kwenye kundi moja kiasilia? Je, uanzishwaji wa Umoja wa Afrika unaangalia tofauti kubwa zilizopo za utamaduni na asili kati ya makundi mbalimbali hapa Afrika kwa nia ya kuboresha sera za muungano huo? Makala hii itaendelea na uchambuzi wa kina zaidi kuhusu hili jambo.


Picha/ramani inapatikana hapa.

No TZ referees ahead of Brazil game



I just came across this DailyNews article about there being no local Tanzanian referees to run the Taifa Stars vs. Brazil game. The match, scheduled to be held in Dar at the National Stadium on Monday, June 7, is highly anticipated by Tanzanians globally.

According to the article, "Tanzania has repeatedly failed to produce quality referees [ in recent decades ] who could make cut in the international scene save for regional tournaments which they have rarely impressed."

There seems to be mounting pressure around this game for those Tanzanians involved in hosting the event. Another DailyNews article discusses why the dates and times changed.

Anyhow, here's what I'm asking: Is this a good time to assess why Tanzania is not in the World Cup or what?

Previous Vijana FM post: Brazil wanakuja kukiputa na Taifa Stars!

(Above image of Collina - even though it has almost nothing to do with this post - courtesy of Rankopedia)